Header Ads

Breaking News
recent

PICHA: MISS WORLD 2013 "MEGAN YOUNG" (MREMBO WA DUNIA) KUTOKA UFILIPINO ATWAA TAJI.

Megan Young - Miss World 2013
 Baada ya Ufilipino kuwa mashuhuri katika tasnia ya Tamthilia nzuri na zenye mahadhi ya kiafrika, sasa yatinga ndani ya Urembo, ikiwa ni baada ya mrembo kutoka nchini humo "Megan Young" kutwaa taji la Miss World 2013 hapo jana.

Shindano hilo la 63 lililofanyika hapo jana katika kisiwa cha Bali nchini Indonesia, ambapo mchuano huo ulikuwa na washiriki 127 ambao walishiriki shindano hilo.

Megan ambaye jana alitwaa taji la mrembo wa dunia kwa mwaka 2013, ana umri wa miaka 23.

Shindano hilo lililofanyika nchini Indoneshi, siku chache kabla ya shindano kufanyika, lilionekana kutishiwa kushambuliwa siku ya mashindano hayo, lakini shambulio hilo halikuweza kutokea kwani pia ulinzi ulionekana kuwa mkali katika eneo la tukio.

Wafilipino wameupokea ushindi huo kwa furaha zisizo na kifani.
Megan Young - Miss World 2013

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.