Header Ads

Breaking News
recent

TAMTHILIA YA “MARA CLARA” EPISODE YA 51 NA 52 – “GARY” AMPIGA RISASI “AMANTE” NA KUWANYOOSHEA BASTORA ALVIRA, SUZAN NA “MARA” KWA PAMOJA.


Njama  ya Gary David  kutaka kuzindua mapenzi ya zamani kati yake  na Alvira, sasa yatinga katika sura ya mbele zaidi, kwani Alvira amkana mumewe Amante mbele ya Gary na kusema hamtaki tena na anataka kuwa na “Gary David”.

Amante kwa kiasi kikubwa anajihisi kama sanamu kwani hakuamini macho na masikio kwa kile alichokisikia kutoka kwa Alvira kuwa hamtaki tena na anamtaka Gary!  Amante kwa sasa anaishi kwa yule bibi aliyekuwa akiwafanyia kazi ambaye Alvira aliamua kumtimua kwa kile alichodai kuwa anaingilia mambo yake binafsi huku akiwa kama kibaraka wa Amante. Bibi huyo anajaribu kurudi kwa Alvira na kumsihi aachane na Gary lakini juhudi hizo zinagonga mwamba.

Alvira anaendelea na uchunguzi wa mauwaji ya Lenita pamoja na mabomu aliyonusulika mwanae MARA. Alvira anafunga safari hadi kwa mama yake Lenita na kumpeleleza kuhusu Lenita, lakini pia juhudi hizo zinagonga mwamba pale mama huyo anapokosa kumuona jambazi aliyekuwa na mwanae Lenita kwani alifanikiwa kumuona siku za nyuma.

Alvira bado anajaribu kumpeleleza mama yake Gary na kumsihi kuwa “najua Mrs. David unampenda mwanao Gary, lakini nikishakamilisha ushahidi nitamrudisha tena mwanao jela”, bibi yuko tayari kutoa siri ya mwanae lakini bado hajaweza kupata muda wa kutosha, huenda akipona kitanuka kwa Gary.

Amante apigwa risasi shingoni, na mtu ambaye huenda akawa Gary, lakini pia mamayake mara aonekana kuwa na dalili za mwanzo za kuwa na ujauzito ambao amehisi ni sikuile ya mwisho ambayo mume wake Gary alimlazimisha wakalala nae ambapo asubuhi yake alitoroka na MARA na kutokomea pasipojulikana.

EPISODE YA 52 GARY AANZA KUMUONYESHA ALVIRA UNYAMA - INAENDELEA HAPA

Baada ya Amante kukosa ushahidi wa kutosha kwa Gary, sasa aamua kumfuatilia katika bishara yake mpya haramu ya dawa za kulevya ili apate sababu ya kumtupa jela Gary. Huku nyumbani kwa Alvira mahusiano yake na Gary yanathibitika baada ya Alvira kutamka mbele ya Amante na Gary kuwa hampendi Amante na bali anampenda Gary peke yake.

Gary anatoa maoni kwa Alvira “nikwanini tusimuondoe Amante duniani ili aache kutuingilia penzi letu?” Alvira anashtuka na kukataa kata kata na kumwambia Gary asijaribu kuingilia na kumdhuru Amante kwani huo ni ugomvi wao, na pia Amante bado ni mumewe wa ndoa. Alvira anaanza kuutambua moyo wa Gary kwa matendo anayoanza kumuonyesha.

Gary anaanza kama kumlazimisha  Alvira wanyonyane ndimi, pia ahamie kwa Alvira, lakini Alvira kwasababu malengo yake sio kuolewa na Gary ni kutafuta vidhibiti vya maovu ya Gary, hivyo anamwambia Gary asiwe na haraka ya mambo, muda utafika tu.

Huko kijijini Suzan anapata vipimo kuwa ni mjamzito, ujauzito unaosemekana kuwa ni wamumewe Gary. MARA adhamilia kabisaa kurudi nyumbani kwao, lakini Alvira anamsihi Suzan amzuie kwani huko mambo  bado sii mazuri. Huku mjini Clara nae amerejea tena huku akiendeleza kumfanyia bibi yake ugaidi.

Mama yake Gary anapata nafuu ya kuweza kutembea japo kwa shida, hadi alikochimbia zile fedha za Gary. Akiwa bado anachimbua, mfanyakazi wake anaanza kumtafuta huku akisaidiana na CG,wanamkuta japo alikuwa bado hajazitoa.

Amante anajipanga yeye na wenzake ili kumfuatilia Gary katika biashara zake za dawa za kulevya, anafanikiwa kuchukua video kwa njia ya simu, lakini wenzake Gary wanashtukia kuwa kunamtu anawafuatilia, hivyo wanamwambia Gary. Amante akiwa bado ananyata kuondoka mara Gary anatokeza kwa nyuma yake na bastora na kusema “Amante leo sitokuacha, huwezi kuondoka”, Gary anampiga risasi na Amante kuanguka chini.

Nyumbani  kwa Gary yeye na Clara wanafanikiwa kuzifukua zile pesa zilizokuwa zimefukiwa na mama yake. Amante afanikiwa kufikishwa hospitali, huku Suzan na MARA wafanikiwa kurudi na kufika hospitali kumuona Amante.

Gary anafika hospitali na kumkuta Suzan na MARA, anatoa bastora na kumnyoshea Suzan lakini Alvira na MARA wanamzingira Suzan kwa pamoja, mara Gary bado akiwa na hasira anawauliza “mnafikiri mtakimbia kwenda wapi?” anawaonyooshea bastora wote watatu. Huku Madaktari wanajaribu kumpiga shoti Amante ili azinduke lakini juhudi kama zinagonga mwamba hivi!, Je nini kitaendelea?

Je nini kitaendelea? Tazama Star TV na karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.