Header Ads

Breaking News
recent

EPISODE YA 50 TAMTHILIA YA “MARA CLARA” – “AMANTE” ATOKA JELA NA KUMFUMA MKEWE “ALVIRA” AKIWA NA “GARY” – ‘ALVILA’ AMFUKUZA “AMANTE”


Familia ya Amante Deville inazidi kusambaratishwa na Gary ikiwa ni baada ya Alvira kumuajiri Gary kuwa kama dereva wake, lakini kumbe kila mmoja ananjama nzito na mwenzake.

Gary anazidi kuongeza ukaribu mkubwa nyumbani kwa Amante ili hali akijua kuwa Amante yuko jela hivyo anatumia nafasi hiyo, kujenga mazoea ya karibu sana na Alvira (mke wa Amante). Lakini Yule bibi ambaye ni msaidizi wa kazi wa nyumbani kwa Amante anaonekana kuwa na wasi wasi na Gary kuajiriwa katika nyumba hiyo.

Bibi anamfuata Alvira na kumtahadharisha kukaa mbali na Gary, lakini Alvira analichukulia swala hilo kitofauti kabisa na kuona kuwa anaingiliwa katika maaamuzi yake binafsi. Siku hiyo hiyo bibi huyo anatoka nje na kumkuta Gary akiwa nafuta gari vumbi na kumuuliza kulikoni yuko pale? Gary anamuelezea kuwa ameajiriwa pale kama dereva, lakini Yule bibi kwakuwa anafahamu ugomvi wa Gary na Amante siku nyingi basi alimuonesha Gary hali ya kutoridhishwa na uwepo wake pale.

Gary anagundua kuwa bibi huyo ndiye anayemshawishi Alvira amfukuze kazi. Gary anajipanga huku usoni akiwa amevaa kininja na kumnyatia  bibi huyo wa kina Amante usiku wakati akitoka kutupa uchafu, anamkaba shingo na kumkandamiza, lakini huko ndani Alvira anahisi kerere nje na kulazimika kuja kumtafuta bibi huyo nje, hapo ndipo alipoachiwa shingo na Gary kutokomea.

MARA huko aliko anaumia mkono baada ya kwenda kuachanisha ugomvi wa Derick (mototo wa boss wao) kijana aliyemuokoa wakati amedumbukia majini. Licha ya MARA kuanza kuzoea mazingira ya huko aliko, kama ameanza kuzoeana na Derick kiaina hivi.

Clara bado yuko kati kati kwani vitendo vya baba yake Gary kuvamia vamia kwa Amante kama vinaanza kumkera hivi, kwasababu siku aliyomkaba Yule bibi, baada ya dakika chache kukabwa, Garl alifika pale nyumbani kwa Amante haraka. Lakini swali moja Yule bibi alimuuliza, ni umejuaje tukio hili limetokea ukaja haraka? Gary alijitetea kuwa, nilipigiwa simu na Clara akihitaji msaada wangu, kiukweli Clara hakupendezwa na hilo lakini kishingo upande ilibidi akubali.

Yule bibi alifunga safari hadi jela na kukwenda kumuambia kilichotokea kwake na akimuomba amzuie mkewe Alvira asimruhusu Gari kuendelea kufanyakazi pale. Siku ya pili Avira anafika jela kumtembelea Amante, lakini amante anaonekana kutokuwa na furaha. Amante anamkalipia na kumuambia amfukuze Gary nyumbani kwake na kusema au wanauhusiano wa kimapenzi na Gary? Alvira anakasilika na kumpiga kofi, mwisho kila mmoja wanaachana wakiwa wamenuniana. Lakini mwanasheria wa Amante anafanikiwa kunasa video ikimuonyesha Gary alivyoenda kumuuwa Christina na hiyo ilisababisha Amante aachiliwe na kurejea nyumbani.

Alvira anamtembelea mama yake Gary aliyepooza nyumbani, akijua kwamba kunakitu bibi huyo hutaka kumuambia kila siku lakini inashindikana. Siku ya kwanza bibi huyo anamuonyesha pesa zilipofukiwa lakini akiwa bado anashangaa mara Gary anawakuta. Siku ya pili bibi anafanikiwa kumuandikia kwenye karatasi neno ”pesa”. Lakini Alvira katika kuificha katika mkoba wake anaidondosha pale chini na kuiacha pale pale. Gary anaikuta na kushtukia mchezo hivyo anamrazimisha mama yake aseme pesa zilipo, lakini pia Alvira amekwisha anza kung’amua kuwa huenda ni zile pesa walizotozwa kwa MARA na CLARA.

Amante anatoka jera na kumkuta Gery akiwa na Alvira nyumbani kwake, aliamini kuwa watu hao walikuwa na mahusiano ya kimapenzi, hivyo alimgombeza mkewe Alvira kwa kitendo hicho.Hiyo haikutosha tuu alimtandika ngumi ya shavu Gary mpaka chini. Alvira anakasilika na kumfukuza Amante. Huko mama yake MARA ashikwa na wasi wasi  kuwa huenda akawa mja mzito, je ujauzito wanani? Je Amante wataachana na mkewe Alvira?.

Je nini kitaendelea? Tazama Star TV na karibu tena kwa dondoo  nyingine za tamthilia hii hapa hapa.

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.