Header Ads

Breaking News
recent

GHOROFA JIPYA LILILO GHARIMU BILIONI 29 LAKABIDHIWA NSSF LEO JIJINI ARUSHA.


DSCN7402Wataalamu wa ujenzi pamoja na wawakilishi wa Shirika la NSSF katika picha ya pamoja mara baada ya makabidhiano ya Jengo kubwa na la kisasa la shirika hilo lililojengwa Jijini Arusha, barabara ya Old Moshi. Jengo hilo lenye jumla ya ghorofa 15, mbili zikiwa chini (basement) kwa ajili ya maegesho ya magari linaelezwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 28.75 na limejengwa kwa muda wa miaka miwili.

Kamapuni ya China Jiangchang Engineering Co. Ltd (CRJE) ndiyo imekabidhi mradi huo ramsi hii leo baada ya kukamilika ujenzi wake uliowashirikisha pia wakandarasi wadogo 6 wa ndani.

 

Jiji la Arusha limepata muonekano mpya kwa kuongezewa jengo refu, kubwa na la kisasa kwa shughuli za kiosifi na biashara. NSSF nao wanategemea kuhamishia offisi zao kwa kanda hii katika jengo hili, halikadhalika huduma za kibenki zitapatikana hapo.
DSCN7392Sehemu ya mbele ya jengo, upande wa kushoto

DSCN7393 
Jengo jipya la Shirika la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (NSSF) lililoko Jijini Arusha, Barabara ya Old Moshi. Jengo hilo limekabidhiwa leo kwa shirika hilo toka kwa mkandarasi kutoka China ambae alishirikiana na wakandarasi wengine wa ndani.

DSCN7376
Mbunifu wa jengo, mwakilishi wa NSSF, Injinia Mshauri pamoja na injinia mkaazi wakipata chakula cha mchana kilichoandaliwa maalumu kwa ajili yao na wataalalmu wengine walioshiriki katika ujenzi wa mradi huo, katika hoteli ya kitalii ya Kibo Palace ya Jijini Arusha.

DSCN7380Wakandarasi wa kichina pamoja na mkadiriaji majengo wa mradi, QS Komba wakiwa katika maankuli.

DSCN7405
Picha na Matukio kwa hisani ya Arusha255 Blog 
na Wazalendo 25 Blog

No comments:

KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.