NI MWAKA MMOJA BAADA YA KIFO CHA GADAFI.
Asili Yetu Tanzania.Copyright

Gadafi wakati wa uhai wake.
Libya inaadhimisha mwaka mmoja baada ya aliyekuwa kiongozi
wa nchi hiyo Muammar Gaddafi kung'olewa madarakani na hatimaye kuuawa.
Kanali Gaddafi alikuwa kiongozi aliyepigania Muungano wa
nchi za Afrika akihimiza ushirikiano miongoni mwa mataifa hayo.
Hata hivyo kumeibuka maswali iwapo mshikamano wa Libya na
mataifa mengine barani Afrika utaendelea baada ya kifo cha Gaddafi.
Gaddafi licha ya kuonekana kama dikteta, lakini pia
alionekana kama mtu anayejali maslahi ya watu wake.
Mmoja wa wananchi wa Libya kutoka kabila la Tuareg Fnayet
Al-Koni, anahisi kuwa utawala mpya wa nchi hiyo lazima uzingatie ushirikiano
mpya na nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, tofauti na uhusiano ambao anautaja
kuwa bandia kati ya Gaddafi na mataifa mengine ya Afrika.
No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA