HUENDA ukawa unadaiwa
madeni mengi na unaona nivigumu kwako kukabiliana nayo moja kwa moja, usiogope
jaribu njia mbadala za kuweza kukabiliana na madeni hapa.Zifuatazo ni baadhi ya
njia zitakazo kusaidia kupambana na ulipaji wa madeni .
1: Tengeneza Orodha yote ya madeni unayodaiwa.
Unapaswa kufahamu
madeni yote unayodaiwa na umjue mtu, kikundi au kampuni inayokudai.Kufanya
hivyo kutakukumbusha kujipanga vizuri katika swala zima la ulipaji.
2: Panga madeni yako kulingana na kiasi, umuhimu na uharaka
wa kuyalipa.
Yapatie kipau
mbele yale madeni uhimu yanayoweza kukuchukulia hatua mara moja.Mara nyingi
madeni haya huwa ni ya kawaida, kwa mfano; kodi ya nyumba, kusimamishiwa huduma
muhimu(maji, umeme) Ada ya shule au hata kwenda jela.Lakini sii lazima uanze tu
na madeni ya aina hii, bali inategemeana na hali iliyopo.
3: Tengeneza bajeti
yako peke yako.
Fanya mahesabu
ili kujua kipato ulichoingiza kwa wiki au mwezi, pamoja na gharama zake zote,
hii itakusaidia sana kuokoa pesa zako.Bajeti itakusaidia kuamua nini unaweza
kumudu kulipa wadai wako, hivyo ni muhimu kuwa mkweli.
4: Kuwa mkweli na muwazi kwa wadeni wako.
Watu wengi
wanafikili kumkwepa mdeni wake ndiyo njia pekee ya kukabiliana na madeni,
hapana! mara nyingi hii hukujengea taswira mbaya katika jamii unayoishi
nayo.Nivyema ukapokea simu ya mdeni wako na kumwambia ukweli na kuomba
akuongezee muda wa kuweza kujipanga zaidi na kufanikisha kulipa madeni yako.
5: Tumia njia ya mazungumzo baina yako na mtu anaye kudai.
Nivyema
ukakubaliana na mdeni wako kias na jinsi ya kulipa deni, nakama ikishindikana
baadaya kuwa umeshakopa, tafuta ushauri kwa wataalam, watakusaidia jinsi ya
kulipa madeni, kwa mfano taasisi binafsi zinazohusika na mikopo katika
jamii.Nivyema ukakabiliana na madeni yako moja kwa moja- kwasababu jinsi
upuuzavyo kulipa madeni ndivyo hali itakavyozidi kuwa mbaya kwako.
NB
Kamwe usikimbie
madeni, jitahidi ukabiliane na madeni kwa kutumia lugha nzuri kwa mdeni wako,
kwasababu madeni humkosesha mtu uhuru, amani na hata pia huhatarisha
maisha.Asante!
No comments:
KARIBU UTOE MAONI YAKO HAPA